Thursday 20 March 2014

Joseph Haule: Dhamira yetu ni kufanya Tanzania iweze kupata Maendeleo kupitia Kilimo

SOTE TUNAAMINI KILIMO NDIO UTI WA MGONGO WA TAIFA LETU!

 Profesa J, ambaye ni balozi wa kampeni hii ya Kilimo Inalipa, Jikite, akisisitiza kwamba kilimo ndio Mkombozi wa Taifa letu la Tanzania

Wadau mbalimbali wa kilimo, wakikubali kwamba sekta ya kilimo inalipa!

Dhamira yetu, nia yetu ni kufanya Tanzania iweze kupata maendeleo kwa kupitia kilimo.

Tunaamini kilimo ndio uti wa mgongo wa Tanzania, kilimo ndio mkombozi pekee wa ajira kwa vijana Tanzania na watu wote. Lakini kilimo ndio ya maendeleo ya msingi kwa ajili taifa letu tukufu la Tanzania.

Sasa nafurahia kuona ANSAF pamoja na ONE wameamua kua na sisi. Nataka kuwaambie kwamba, kuna mmoja kati ya wachangia hoja hapa amesema vijana wanakimbia kijijini kwenda mjini lakini ajira zipo kulekule kijijini.

Tuna ardhi nzuri yenye rutuba na tumebarikiwa kuwa na nafasi, nyie mnaweza mkashiriki kwa kuona sasa hivi Iringa mvua zinanyesha.Tuna ardhi iliyotukuka sana, tuigeuze na tuamue  kufanya kilimo kama mkombozi wa Tanzania.

"Nafurahi sana, najiona nimebalikiwa sana sana kua part and parcel kwenye kampeni hii ya kufanya kilimo kuwa mkombozi kweli wa Mtanzania", alisema Profesa J.


Dokii, Profesa J na Mrisho Mpoto wakifatilia mjadala kwa makini

Wadau mbalimbali wa kilimowakisikiliza kwa makini
 Profesa J (Katikati) akielezea ujuzi wake katika sekta ya Kilimo, Kulia ni Mrisho Mpoto na kushoto ni Masoud Kipanya-mabalozi wa kampeni hii ya Kilimo Inalipa, JIKITE!



No comments:

Post a Comment