UKIWA MKULIMA UNAUWEZO WA KULISHA NA KUWA TAJIRI
Masoud Kipanya akizungumza na wakulima
Mercy, Mwakilishi kutoka Shirika la ONE katika mazungumzo yake alisema kwamba tajiri mkubwa wa afrika anaitwa Dangote ni mkulima, maana yake nini?
Maana yake Dangote sio kwamba analima hewani ila anafanya taratibu zote kama sisi tunavyofanya. Yeye anaishi Nijeria, ardhi iliyopo huko ni sawa na iliyopo Tanzania tena inawezekana Tanzania ikawa na maeneo mazuri zaidi.
Sisi kama binaadamu tunaweza kua mabilioni, kwa sababu binaadamu anaweza kuacha vitu vyote lakini chakula ni lazima ale, sasa kuna biashara kubwa zaidi ya kuzalisha chakula? Hakuna.
Ukiwa mkulima unanfasi kubwa ya kulisha jamii lakini vile vile na kutajirika.
Kipanya akisisitiza umuhimu wa kilimo
Mimi kama Masoud Kipanya
nina miradi miwili ambayo ninaifanya.Wa kwanza ni Maisha
plus-kipindi cha televishen sasa hivi tunawaganisha vijana pamoja na
wakina mama wazalishaji wa chakula. Nia yetu kubwa ni kuwaambukiza hawa vijana
ili hii tabia ya kutoroka kutoka vijijini kukimbilia mijini iweze kuisha, watu
waweze kujua namna wanavyoweza kutembea juu ya hela wakiwa kijijini .
Mradi wa pili tunaufanya
na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, ambapo tuna vijana 100 tumewaweka porini kwa kufuata
model ileile ya maisha plus. Wale vijana 100 tumeanza kukaa nao tangu mwaka
jana (2013) mwezi 4 na wanafanya kilimo cha hali ya juu kabisa. Hata mimi
mwenyewe mjini nimeanza kuhama kabisa utanikiuta Tabora. Dar es salam tunaacha
AC, magari mazuri kwa sababu tunajua tunakoelekea.
Mwaka huu vijana wamelima
hekta 20 za tumbaku lakini vile vile wanalima na mahindi. Mwakani wanatarajia
kulima hekta 100 kwa hivyo kuna unawezekano wa kutengeneza milioni 700 au 800
ni mkubwa sana. Sasa unasemaje kuhusu
kilimo?
Masoud Kipanya akiwa na mabalozi wenzake, Profesa J na Mrisho Mpoto
No comments:
Post a Comment