Thursday 13 March 2014

KATIKA KUAZIMISHA MWAKA WA KILIMO WA AFRIKA, ANSAF YAZINDUA KAMPENI YA KILIMO INALIPA, JIKITE.





                     Mkurugenzi Mtendaji wa ANSAF, Audax Rukonge

Jukwaa la Wadau wa Kilimo (ANSAF), limezinduzi wa Mwaka wa Kilimo barani Afrika, uliotangazwa 2012 na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) Rais Thomas Yayi Boni. Kwa Tanzania Uzinduzi huo ulifanyika katika kijiji cha Kaning'ombe Mkoani Iringa.
"kwa muda mrefu sasa jamii imekua ikiamini na kutafsiri kilimo kwa mtazamo hasi, hivyo kushindwa kuzitambua fursa zinazotokana na sekta hio".Bwana Rukonge aliyasema hayo  na kuitaka jamii iachane na kasumba ya kuona sekta ya kilimo kuwa ni ya watu walioshindwa kufanikiwa katika maisha, wazee ama wastaafu katika utumishi wa umma. Badala yake wametakiwa kutambua umuhimu wa kilimo katika kutoa fursa zinazochangia ukuaji wa uchumi na kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira nchini.


Nae mwakilishi wa taasisi ya ONE kutoka Afrika Kusinu Mercy Erhiawarien alisema nchi za Afrika zinapaswa kutekeleza Azimio la Maputo kwa Mwaka 2003 kuhusu kilimo. Kati ya nchi 53 ni nchi nane zimefanikiwa kutekeleza azamio hio, Kampeni ya ‘Kilimo Inalipa, Jikite’ inalenga kuwahamasisha watoa maamuzi, watunga sera na wadau wa kilimo kubadilisha kilimo huku fursa zaidi zikitolewa kwa wanawake na vijana.


Kwa upande wa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Iringa  Dk. Christine Ishengoma aliwaasa wakulima kutumia kwa usahihi mbolea za kukuzia mazao, huku akithibitisha kwamba serikali katika ngazi tofauti inazifanyia kazi changamoto zinzowakabili wakulima kuhusu pembejeo.



Uzinduzi wa Mwaka wa kilimo pamoja na kampeni ya Kilimo Inalipa, Jikite ilipambwa na vikundi vya ngoma

















No comments:

Post a Comment